Monday, 21 April 2014

ASKOFU MACHA WA JCMI ARUSHA ATUMIA IBADA YA PASAKA KUWAASA WAKRISTO JUU YA AMANI YA TANZANIA PAMOJA NA BUNGE LA KATIBA.






                              Askofu Paulo  Macha

Askofu wa makanisa ya JCMI Arusha Bishop Paulo Macha ametumia siku kuu ya pasaka kuwaasa waumini wa makanisa ayo kuombea amani ya Tanzania pamoja na bunge la katiba linaloendelea mkoani Dodoma.


Bishop Paulo macha ameyasema ayo wakati akifundisha neno  la mungu kanisani hapo na kusisitiza waumini kuwa na moyo wakuliombea Taifa kwani Amani ya nchi imebadirika ikiwa tofauti na zamani kwani matukio mengi yasiyotegemewa yanajitokeza na kuashiria kupotea kwa amani nchini.



                 Waumini wa JCMI wakimsikiliza Askofu kwa umakini

“Ivi sasa baadhi ya makanisa mengi mkoani Dar es salaam yamebidi kuwekewa ulizi wa polisi kutokana na kuhofia mlipuko wa mabomu unaojitokeza mara kwa mara na kuashiria kua amani imepotea Tanzania”Alisema Macha.
Aidha ameongeza kua Mkoa wa Arusha ndio unaongoza kwa matukio mengi ya ulipukaji wa mabomu na kusababisha vifo vya watu hivyo waumini wanapaswa kutumia mda mwingi kufunga na kuombea mkoa wa Arusha pamoja na Taifa kwa ujumla ili amani isipotee.

            Pastor Steven Wambura kutoka Dar es salaam     
                    akizungumzia amani ya Tanzania.
“Bungeni nako kumekua na mvutano  mkubwa katika uundajii wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na kusababisha mgawanyiko mkubwa kati ya wabunge vyama vya upinzani na chama tawala na kusababisha ugumu wa kupata katiba ya Nchi hivyo waumini tunapaswa kusimama kwa makini kuliomba bunge letu”Alisema macha.



No comments:

Post a Comment