Tuesday, 15 April 2014

MKE WA MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI ALIYEFARIKI NCHINI KENYA AJIFUNGUA MDA MCHACHE BAADA YA MAZISHI YA MUMEWE

Marehemu Peter Kaberere na mkewe enzi za uhai wake.

Mke wa mwimbaji wa muziki wa injili nchini Kenya marehemu Peter Kaberere ambaye amefariki wiki iliyopita wakati akiosha gari yake, mkewe amejifungua mtoto wa kike masaa machache baada ya mazishi ya mwimbaji huyo siku ya ijumaa iliyopita.

Mke wa marehemu aitwaye Mary Njeri au wengi hupenda kumwita Njesh alikuwa mjamzito wa kukaribia kujifungua wakati mmewe alipofariki wiki iliyopita. Tayari wanandoa hao walikuwa na mtoto wa kiume kabla ya baraka nyingine ya mtoto wa kike ambaye amezaliwa wakati ambao mwimbaji huyo ameshaaga dunia

No comments:

Post a Comment