Tuesday, 12 August 2014

MFALME EDWARD ATANGAZA SIKU 10 ZA UKOMBOZI JIJINI ARUSHA NI KATIKA KANISA LA JCMI MOROMBO KUANZIA AUGUST 13.

MFALME EDWARD
 Mtumishi wa mungu Mfalme Edward ametangaza siku 10 za ukombozi jijini Arusha kwa kutoa semina ya neno la mungu itakayofanyika katika kanisa la JCMI ARUSHA lililopo kwa moromboo mwisho wa hiace kuanzia Tarehe 13/08/2014 mpaka tar 24/08/2014 saa 9 mchana mpaka saa 12..Watu wengi wameponywa kupitia maombia na wamefunguliwa kutoka vifungo mbalimbali
           Askofu wa makanisa ya JCMI ARUSHA  PAUL MACHA(pichani) atakuwepo kukuombea kwenye semina iyo..
                           JIONEE HAPA CHINI USHUHUDA WA WATU WALIOPONYWA

Monday, 11 August 2014

PICHA KAMILI UZINDUZI WA ALBUM YA KAMATA PINDO LA YESU YA ROSE MUHANDO JIJINI DAR ES SALAAM,,WAZIRI MSTAAFU AONYESHA USHIRIKIANO..

Angalia picha mablimbali za uzinduzi wa album ya malkia wa muziki wa injili nchini Rose Muhando iitwayo 'Kamata pindo la Yesu' iliyofanyika jumapili iliyopita katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam, chini ya Msama Promotions mgeni mwalikwa akiwa waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya tatu mheshimiwa Fredrick Sumaye. Ukitaka kuangalia video za namna uimbaji ulivyokuwa siku hiyo .

Jessica BM na kundi lake wakimsifu Mungu.
Haya sasa mambo yalinoga zaidi kama uonavyo.

Tuesday, 22 April 2014

PICHA ZA AWALI ZA TAMASHA LA PASAKA JIJINI DAR ES SALAAM...ROZI MUHANDO NA MASANJA NA WALIFANYA VIZURI.

  Karibu tukupe picha za awali za tamasha la kimataifa la Pasaka kama ambavyo huwa linaandaliwa na kampuni ya Msama Promotions. Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake vilipata fursa ya kumsifu na kumuabudu Mungu kwa uimbaji, wakiongozwa na waimbaji nyota barani Afrika. Kekeletso Phoofolo akiwa nahodha.
 Kama kawaida ilikuwepo kwa ajili yako, kama ulitamani kuja lakini hukufanikiwa, pengine ulikuwa 'Canada' au 'Benin', basi picha hizi ni za awali, endelea kutembelea kwa ajili ya picha kedekede za ziada na hata video za tukio hilo. Kama ulikuwepo, basi na tujikumbushe na kisha utuandikie maoni ni muimbaji gani alikugusa sana kwenye tamasha hilo.
Ni mwendo wa mfululizo, wimbo hadi wimbo. Prophet Keke punde baada ya kupanda jukwaani

Monday, 21 April 2014

ASKOFU MACHA WA JCMI ARUSHA ATUMIA IBADA YA PASAKA KUWAASA WAKRISTO JUU YA AMANI YA TANZANIA PAMOJA NA BUNGE LA KATIBA.






                              Askofu Paulo  Macha

Askofu wa makanisa ya JCMI Arusha Bishop Paulo Macha ametumia siku kuu ya pasaka kuwaasa waumini wa makanisa ayo kuombea amani ya Tanzania pamoja na bunge la katiba linaloendelea mkoani Dodoma.

Tuesday, 15 April 2014

MKE WA MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI ALIYEFARIKI NCHINI KENYA AJIFUNGUA MDA MCHACHE BAADA YA MAZISHI YA MUMEWE

Marehemu Peter Kaberere na mkewe enzi za uhai wake.

Mke wa mwimbaji wa muziki wa injili nchini Kenya marehemu Peter Kaberere ambaye amefariki wiki iliyopita wakati akiosha gari yake, mkewe amejifungua mtoto wa kike masaa machache baada ya mazishi ya mwimbaji huyo siku ya ijumaa iliyopita.

SOMO LA LEO : KIPIMO KIKUBWA CHA MTU MKAMILIFU ..

NENO LA MSINGI:

YAKOBO 3:2:

“Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. MTU ASIYEJIKWAA KATIKA KUNENA, HUYO NI MTU MKAMILIFU, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.”

<><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><

Viko vipimo kadhaa katika Biblia ambavyo tunaweza kujipima ukamilifu wetu, huku tukijilinganisha na mfano wa mtu mkamilifu, Yesu Kristo [ZABURI 37:37]. Kipimo kikubwa kimojawapo cha ukamilifu ni mtu kuweza kuuzuia na kuutawala ulimi; na kuufanya useme yale tu ambayo Yesu mwenyewe angeweza kuyasema. Biblia inasema kwamba, ulimi wa mtu asiye mkamilifu ni ULIMI MOTO NA ULIMWENGU WA UOVU; nao ndio uutiao mwili wote unajisi, na kuuwasha moto mfulizo wa maumbile [YAKOBO 3:6]. Ikiwa watu wengi katika Kanisa la Nyumbani au Kanisa Kuu, ndimi zao ni moto na ulimwengu wa uovu; basi mwili wote yaani Kanisa lote litatiwa unajisi na kuwashwa moto kwa sababu yao. Moto wa ulimi unaweza kuligawanya Kanisa, na kuleta makundi makundi kuondoa upendo kati yetu na kumfanya Roho Mtakatifu awe mbali nasi. Biblia inasema “Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo[YAKOBO 3:10]. Biblia inazidi kutueleza kwamba, mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, dini yake mtu huyo haifai na anajidanganya moyo wake kwamba ni mkristo [YAKOBO 1:26]. Ikiwa tunataka kufahamika kwamba ni wakristo, basi inatubidi tuwe na ndimi zilizo baridi, zinazotoa baraka wakati wote katika Kanisa, na mataifa wanaotuzunguka.

Friday, 11 April 2014

MTOTO ALIYEPIGWA RISASI YA KICHWA KANISANI, APEWA RUHUSA YA KUTOKA HOSPITALINI BAADA YA MATIBABU

Mtoto Satrine akiwa na baba yake hapo jana, baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini ©mobile.nation
Hatimaye mtoto wa mwaka mmoja na nusu Satrine Osinya ambaye risasi ilituhama kichwani kwake baada ya tukio la mtu asiyefahamika kuvamia kanisa mjini Mombasa na kufyatua risasi na kuua watu wawili eneo la tukio na wengine wanne baadae akiwemo mama mzazi wa mtoto huyo, hapo jana ameruhusiwa kutoka hospitalini alikokuwa chini ya uangalizi wa daktari baada ya kutolewa risasi hiyo.

Friday, 14 March 2014

HUYU NDIYE MUIMBAJI ALIYENUSURIKA UPASUAJI KWA KALENDA YA MUNGU


Anastazia Mukabwa katika mojawapo ya matamasha mjini Arusha.
Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu

RAIS WA KOREA KASKAZINI AAGIZA WAKRISTO 33 KUNYONGWA


Rais Kim Jong Un wa Korea Kaskazini.©Manlycurls
Wakristo duniani wametakiwa kuomba kwa ajili ya mabadiliko ya ki Mungu katika taifa la Korea Kaskazini ambako Rais wa nchi hiyo Kim Jong Un ameagiza kunyongwa kwa wakristo wapatao 33 wa nchini humo ambao wanadaiwa kupokea msaada wa kuendesha makanisa ya siri kutoka kwa mmisionary wa Korea ya Kusini Kim Jong Wook.

SOMO : KUHARIBU MAZAO YA NDOA ZA KISHETANI / KICHAWI


Tulijifunza wiki iliyopita kwamba kuna majini yanaoa watu kwenye ulimwengu wa roho au ndotoni. Ndoto ni bayana watu wote walioota ndoto zilikuwa kweli. Mfano,
- Yakobo aliota ndota ikawa kweli,
-mfalme aliota ndoto ikawa kweli
- mamajusi wa mashariki waliota ndoto ikawa kweli

NDEGE YA MALAYSIA IPO CHINI YA MAJI BAHARINI WATAIPATA HIVI KARIBUNI,,TB JOSHUA ANENA"

“The plane concerned is deep inside the sea. Some of the particles will be seen on the surface of the sea any moment from now.May their souls rest in peace. We pray the Lord gives the family and loved ones the strength to bear the loss. Our prayer and love are always with them, the nation of Malaysia and other countries who had passengers on this flight.”However,US Counter-terrorism officials now suspect that the plane flew for a total of five hours based on data automatically downloaded and sent back to Rolls Royce - the manufacturers of the Boeing 777's engines.
They are now pursuing the astonishing possibility that the plane and its 239 passengers was diverted to an undisclosed location 'with the intention of using it later of another purpose.The pilot or somebody else turned the planes' transponders off to avoid detection and flew it to another location

KICHANGA CHAFUFUKA DAKIKA 28 BAADA YA KUZALIWA MFU

Kuna msemo unasema, uchungu wa mwana aujuyae mzazi. Hapa pia niseme uchungu wa kujifungua, aujuaye ni mama. Na furaha ya ufufuo anaijua hasa aliyefiwa. Tukio mojawapo lililotokea nchini Canada, ambapo mama wa watoto watatu, alikuwa anatarajia kupata mtoto wake wa nne, binti - lakini hali ikawa tofauti siku hiyo.

Saturday, 8 March 2014

SOMO : WANAUME AU WANAWAKE WA ROHONI (MAJINI MAHABA) NA JINSI YA KUWASHINDA.

Biblia inasema, Wakorintho 6:16;
‘...Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. 17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye..

Wednesday, 5 March 2014

MAKALA: KAMA HUJAFELI BASI HUJAJARIBU, NA USIPOJARIBU HUWEZI KUFANIKIWA


Mgunduzi wa taa, Thomas Edison alijaribu zaidi ya mara 1000 hadi akafanikiwa.
                          Kwa maisha ya hivi sasa, ni habari ya kuchakarika kwa kwenda mbele. Sizungumzii wale wanaojipatia mali kwa njia iliyopinda, mathalani utapeli, wizi, na hata ujambazi wa kalamu na mwili, la hasha. Nazungumzia kuchakarika kwa mtu kudamkia kazi mapema iwezikanavyo, kabla hata ya wengine hawajamaliza ndoto zao.

Tuesday, 4 March 2014

ASKOFU PAULO MACHA AKAMATA VIFAA VINAVYOSADIKIWA KUTUMIWA NA WACHAWI NA KUVITEKETEZA NA MOTO.

 Askofu Macha akiwaonyesha waumini wa kanisa la JCMI  wakati wa ibada  vitu vinavyosadikiwa kua ni vya kichawi vilivyotolewa kwenye nyumba ya mtu(jina tunalihifadhi)na hatimye mtu huyo kuamua kuokoka na kachana na mambo ya kishirikina.

AFUNGULIWA KUTOKA KATIKA UKICHAA BAADA YA MAOMBEZI


Dada huyu alifikishwa katika hospitali mojawapo jijini hapa (jina tunalihifadhi); kwa bahati nzuri katika hospitali hiyo kulikuwa na nesi ambaye ameokoka na yupo Ufufuo na Uzima.

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI ROSE WILLIAMU ATOA USHUHUDA BAADA YA KUPONA UKIMWI.soma hapa kujua zaidi

Mwimbaji wa nyimbo za injili Rose williamu ametoa ushuhuda wa kupona ukimwi  aliokaa nao wa mda mrefu kupitia maombezi ya Askofu wa kanisa la  JCMI Arusha Paulo Macha kumfanyia maombezi na atimaye kupona kabisa virusi vya ukimwi na sasa ni mzima wa afya.

Thursday, 27 February 2014

MKOA WA IRINGA WATIKISWA KATIKA PASAKA 2013 NA UIMBAJI WA ROSE MUHANDO

Rose Muhando alikuwa gumzo mjini Iringa kwa uimbaji wake. Mkoa wa Iringa ulifurahishwa na huduma ya mwimbaji huyu. Watu walifurika uwanjani mapema kuangalia kitimutimu cha waimbaji wa nyimbo za injili akiwemo Malkia wa Muziki wa Injili Tanzania Rose Muhando.